Wanawake watano wachomwa moto hadi kufa

Watu watano wameuwa kwa kuchomwa moto katika kata ya Uchama Wilayani Nzega Mkoani Tabora na watu wanaosaidikiwa kuwa ni Sungusungu huku wakidaiwa wameuwawa kutokana na imani za kishirikina.
Kufuatia Mauaji hayo Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Agreya Mwanri, amezitaka Kamati za Ulinzi na usalama ngazi ya Mkoa na ile ya Wilaya ya Nzega kusitisha shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na sungusungu katika kijiji hicho.
Mwanri amesema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya sungusungu hao kutekeleza mauaji hayo ya watu watano ambao wote ni wanawake wakituhumiwa kuwa ni washirikina.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa katika kuendelea kuchunguza tukio hilo jeshi hilo linawashikilia baadhi ya viongozi wa kijiji hicho ili kuweza kubaini waliotekeleza tukio hilo.

from Blogger http://ift.tt/2h5S8ia
via IFTTT