MWANAMUZIKI Chid Benz Amshushia Mkwala Mzito Chin Bees…

Msanii wa hip hop Bongo, Chid Benz amemtaka msanii mwenzake Chin Bees kutafuta jina lingine.
Sababu ya Chid Benz kusema hivyo imetokana na majina yao kufanana, na kuongeza kuwa wote wanafanya muziki wa aina tofauti hivyo kulikuwa hakuna ulazima wa ufanya hivyo.
“Siku moja nimeona Shetta anamuangalia instagram nikamuuliza huyo ni nini?, akaniambia ni Chin Bees, nikamuuliza anafanya muziki gani, akaniambia Bongo Fleva!. Sisemi kwa ubaya ila sikuelewa ile style anayofanya yeye ni tofauti sana na mimi mtu mzima mwenye hit kama 32 najua nikiingia kwenye stage nachapa tu,” Chid Benz ameiambia Planet Bongo ya EA Radio na kuhoji.
“Huyo Chin Bees ana single hata saba kweli?, atafute jina lingine,” amemaliza kwa kusema.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sI7dan
via IFTTT