Wema Sepetu Amzimikia Rayvanny Amtabiria Makubwa Tuzo za BET

RayVanny ni msanii pekee kutoka Tanzania na Afrika Mashariki ambaye anatuwakilisha kwenye tuzo za BET zitakazofanyika Marekani baadaye mwezi huu akiwania Viewers Choice Awards ama (Pendekezo la Mashabiki ama watazamaji) huku BET wakitangaza namna ya kuwapigia kura wasanii ili washinde tuzo hizo.
Pamoja na baadhi ya mastaa kama Elizabeth Michael kumpigia na kumuombea kura RayVanny kwenye kurasa zao za Social media, Wema Sepetu naye ametumia ukurasa wake wa Instagram kumpigia kura RayVanny akiandika:

Umechaguliwa tu kuwania lakini kwangu wewe ni mshindi tayari …Unastahili kabisa! V-Vanny Boy. Na haiishii hapa Tuendelee kupiga kura.

 Wasanii wanaowania tuzo ya Viewers Choice Awards pamoja na RayVnanny ni pamoja na Dave (UK ) Jorja Smith (UK) Amanda Black (South Africa) Changmo (South Korea) Daniel Caesar (Canada) Remi (Australia) Skip Marley (Jamaica).
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t1Uobm
via IFTTT