Utata Waibuka Juu ya Sehemu ya Kuuaga Mwili wa Ndesamburo..Lema Afunguka Haya Mazito Kuhusu Njama za Jeshi la Polisi Kuzuia Tukio Hilo..!!!

Mbunge wa Arusha mjini, Mh. Godbless Jonathan Lema amedai Vyombo vya usalama vimezuia kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Moshi mjini Mh. Philemon Ndesamburo kwenye uwanja wa Mashujaa.
Kupitia ukurasa wake wa twitter Mh. Lema amedai kuwa amezungumza na Diwani wa kata ya Sombetini Mh. Ally Bananga na kwamba wamezuiliwa na vyombo vya usalama kufanyia hapo shughuli ya kumuaga Mzee Ndesamburo.
“Nimeongea na Mh Bananga aliyeko uwanja wa mashujaa , vyombo vya usalama vinazuia kuaga mwili wa Ndesamburo kuagwa hapo. Hii ni mbaya sana” – Mh. Godbless Lema.

from Blogger http://ift.tt/2qTUQqJ
via IFTTT