Soko la usajili ‘kichaa’ linavyoipa Man United wakati mgumu kukamilisha usajili wake

Wakati Jose Mourinho na boss wake Ed Woodward walihitimisha listi ya wachezaji wanaotaka kuwasajili katika dirisha hili la usajili, walifahamu fika kwamba dirisha hili la usajili litakuwa gumu.
Huku kukiwa na mapato ya £8.3 billion wanayogawana timu 20 za premier league zinazotokana na mauzo ya haki za mtanagazo ya TV duniani kote, pamoja na uwekezaji mpya wa wamiliki wapya vilabu nyumbani na nje ya Uingereza – ushindani wa kusaini wachezaji lazima ungekuwa mgumu sana. 
Sasa, mwezi mmoja ukiwa umekamilika tangu dirisha la usajili liwe wazi, wasiwasi wa Mourinho na Woodward umekuwa ukweli – soko la usajilo limekuwa gumu sana kwa timu nyingi. 
Kwa United, angalia jitihada zao za kumsaini kiungo wa ulinzi. United walikuwa wanaangalia kumsaini Eric Dier lakini pamoja na kwamba wana uwezo wa kumlipa mara 2 zaidi ya mshahara wake wa sasa, Spurs bado wameweza kugoma kumuuza kwa bei ya kawaida na wameamua kubaki nae – yote haya wakiyafanya huku wakiwa wanajenga uwanja mpya unaowagharimu kiasi cha £800 million.
Jose Mourinho alipohojiwa na jarida la France Football mwezi March kwamba United wanaweza wasifanikiwe kupata mchezaji kutoka Tottenham au timu nyingine yoyote ya Top 6 ya Premier League na sasa inaonekana huenda jambo hilo linaweza lisiwezekane katika timu 10 za juu za EPL – kila timu ina pesa na hivyo inakuwa ngumu kuuziana wachezaji kwasababu kila inataka kujiimarisha.
Nemanja Matic anaweza kuwa na upekee kwenye hili kwasababu Chelsea wana utayari kumuachia mserbia huyo ikiwa watafanikiwa kupata saini ya Tiemoue Bakayoko kutoka Monaco. Ikiwa dili hizi mbili za usajili zitakamilika, Chelsea wanaweza kumbadili kiungo mwenye umri wa miaka 28 kwa mwenye umri wa miaka 22 na bado watatengeneza faida ya £5m. Wakati huo huo Mourinho atampata kiungo ambaye anamfahamu vyema, ambaye anaifahamu vyema EPL na kuimudu na ameshaisadia Chelsea kushinda vikombe viwili vya premier League katika kipindi cha miaka 3 iliyopita.
United walikuwa wamepanga usajili wa wachezaji 4 ukamilike kabla ya wachezaji wote kurejea Carrington mnamo July 8, takribani wiki moja na nusu kutoka sasa. 
Lindelof tayari amewasili, hata hivyo uhamisho ulianza kujadiliwa na pande mbili za United na Benfica kutokea mwezi December 2016, ingawa uhamisho wa January ulisitishwa, lakini uliweka mazingira mazuri ya dili hili kukamilika kipindi hiki cha usajili. 
Woodward na timu yake wanapambana dhidi ya timu pinzani ambazo kwa mujibu ya walio ndani ya Old Trafford, wapinzani wao wanakuwa kiuchumi kila mwaka
Mfano Everton, hawajawahi kutazamwa kama wapinzani tangu miaka 1980 lakini hivi sasa kwenye dirisha hili la usajili wameshatumia zaidi ya £55m kwa wachezaji wawili tu – Jordan Pickford kwa £30m na Davy Klaassen kwa £25m. Pia wanakomaa kumruhusu Romelu Lukaku kuondoka isipokuwa timu inayomtaka itakapolipa £85m. Wachambuzi wa mambo ndani ya United wanaamini Everton walioshika nafasi ya 7 msimu uliopita wanaweza kuingia Top 4 msimu ujao ikiwa watafanya usajili mzuri na kubaki na Lukaku kwenye kikosi chao. 
Upande mwingine, vilabu vya nje AC Milan na Inter Milan wana uwekezaji wa matajiri kutoka China. Inter mpaka sasa wameendelea kuisumbua United na kugoma kumuuza Ivan Perisic mpaka United itakapolipa kiasi cha €50m, pamoja na kwamba wanahitaji kukusanya kiasi kichopungua €30m mpaka kufikia Ijumaa hii ili kuepukana na adhabu za kukiuka sheria ya Financial Fair Play. United sasa hawapambani na wakubwa wenzao tu kama Barcelona, Real Madrid, City, Bayern Munich na Chelsea. 
Mourinho alisema hadharani kwamba amemwambia Woodward asijisumbue kuhangaika na usajili wa wachezaji wasiouzika kirahisi na timu zao. Bila kuwataja majina, ilionekana wazi alikuwa akiwazungumzia akina Neymar, CR7, na wengineo wa aina hiyo ambao United imekuwa ikihusishwa nao kila wakati wa usajili. Hata dili za usajili za wachezaji aina ya Dier na Perisic – huko nyuma zilionekana rahisi lakini sasa nao wanaingia kwenye kundi la wachezaji wagumu kusajiliwa. 
Watu kadhaa wanaohusika na biashara za usajili , mawakala, washauri wa biashara, wanasheria, wamekaririwa wakisema soko la usajili limekuwa ‘kichaa’ na hata United wenye sifa ya kuwa klabu tajiri duniani nao wanaiona hali ilivyo ngumu katika kukamilisha uhamisho wa wachezaji kama zilivyo timu nyingine. 
Hii ndio sababu mojawapo katika dirisha hili la usajili wakamsaini mbobezi wa masuala la usajili na mikataba ya wachezaji, Javier Ribalta, ambaye ana sifa kubwa aliyojitengenezea akiwa Juventus. Woodward na Mourinho walitabiri soko gumu la usajili, lakini inaonekana hata wao hawakutegemea kutakuwa na ugumu wa namna hii, na hii ndio sababu mpaka sasa dirisha hili la usajili linaonekana kupooza kwa kutokamilika kwa usajili wa wachezaji wengi mpaka tunaingia mwezi July.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2umtYlm
via IFTTT