Hili lingine la Rayvanny na BASATA Kuhusu Mapokezi na Tuzo ya BET

Siku moja baada ya mwimbaji Rayvanny kuwasili Bongo na kukutana na mapokezi makubwa Airport DSM akiwa na tuzo yake ya BET akiwa msanii kwanza wa Bongofleva kutwaa tuzo hiyo…story gumzo ni kuhusu kutooneakana mwakilishi wa BASATA Airport.
255 ya XXL ya Clouds FM leo June 29, 2017 imempata Katibu Mkuu wa BASATA, Godfrey Mngereza ambaye ameelezea sababu za kutoonekana mwakilishi wa Baraza hilo akisema kulikuwa na mawasiliano finyu kati ya Rayvanny na BASATA wakati anakwenda na kurudi kuchukua tuzo hiyo.

“Hakukuwa na mawasiliano mazuri alivyokuwa amekwenda na ujio wake lakini tungekuwa tunaifahamu ratiba yake Baraza kama ilivyo ada huwa hatuna budi ya kwenda kumpokea Airport, kwanza inaleta heshima.

“Kwa hiyo, hakuna sababu ya kusema tusingeenda kumpokea ni kwamba mawasiliano hayakuwepo tangu anaenda na pia ningependa nikumbushe wasanii wanavyokwenda nje ya mipaka ya Tanzania ni vizuri tukaagana ili tukajua ratiba ikoje hata wakirudi tuwapokee.” – Godfrey Mngereza.

Wakati huo huo Rayvanny amefunguka akidai kuwa sasa hivi kila kitu kipo wazi kutokana na mitandao lakini pia BASATA walitakiwa kusoma chochote kipindi tu walipoona amechaguliwa kwa kuwa ndio wazazi wa muziki wa Bongofleva na kama viongozi wao walipaswa kutoa support.
“Kwa mafano, mimi nilivyochaguliwa kam BASATA walikuwa wameona. Wao ni wazazi walikuwa na chochote cha kusema lakini wakisema kwamba wanasubiri niende mimi mwenyewe au tunasubiri watuambie au hatuwezi kwenda kwa sababu hatujaambiwa. Wale ni wakubwa kwetu ni wazazi wetu tunategemea kwamba wanakuza sanaa yetu na sisi tunawaangalia wao walitakiwa kuwa kipaumbele sisi kutusaidia.” – Rayvanny.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sYboSX
via IFTTT