Fundi Mbao Atiwa Mbaroni kwa Kubaka Watoto Wake Wawili wa Kuzaa..

FUNDI mbao, Japhet Lendiman (38) mkazi wa Daraja Mbili, anashikiliwa na Jeshi la Polisi, baada ya kubaka watoto wake wa kike wa darasa la sita na kidato cha kwanza.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini kiini cha tatizo hilo ni nini na kufuatiwa na hatua ya kufikishwa mahakamani. Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na Jeshi la polisi tangu Juni 6, mwaka huu na upelelezi unaendelea kubaini undani wa tukio hilo.
Akimzungumzia mtuhumiwa huyo, mmoja wa majirani wa eneo hilo la Daraja Mbili (jina limehifadhiwa) alidai kuwa mzazi huyo amezoeleka kwa tabia hiyo mbaya mtaani kwao. Alidai kuwa mtuhumiwa huyo amezoea kubaka watoto wake mara kwa mara wakati mama yao akiwa kazini na kwamba Mei 28 majira ya saa 9:00 alasiri alimbaka tena mtoto wake (Jina tumelihifadhi) wa darasa la sita shule ya Msingi Daraja Mbili ndipo taarifa zilipoanza kuzagaa mtaani.
“Siku hiyo ya tukio lililosababisha mzazi huyo kukamatwa mtoto aliona sasa uvumilivu umefika mwisho, alikwenda kwa mama mkubwa na kutoa taarifa jinsi baba yake anavyomwingilia na kueleza kuwa anataka kunywa sumu ili afe,” alieleza jirani huyo. Alisema baada ya maelezo hayo mama mkubwa aliamua kuhoji watoto wote wa shemeji yake akiwemo mwingine wa umri wa miaka 14 (jina limeifadhiwa) ambaye yupo kidato cha Kwanza Sekondari ya Felix Mrema, alikiri kuingiliwa na baba yake tangu mwaka 2016. Aliendelea kueleza kwamba mama yao mkubwa ambaye ni muuguzi (jina limehifadhiwa ) katika moja ya hosptali mkoani Arusha, aliamua kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa mtaa na Polisi.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sUllOT
via IFTTT