Andre Silva atimkia Ac Milan.

Kati ya vilabu vinavyofanya balaa kubwa sana klatika msimu huu wa usajili ni Ac Milan na wanaonekana wamepania sana kurudisha heshima yao iliyopotea kwa miaka kadhaa sasa kwa kununua wachezaji wakubwa.
Leo klabu hiyo imetawala vichwa vya habari baada ya kumnunua moja kati ya washambuliaji waliokuwa wakisakwa na vilabu vingi msimu huu Andre Silva, mshambuliaji huyo amesaini Ac Millan kwa dau la euro 38m akitokea klabu ya Fc Porto.
Msimu ulioisha Silva alifunga jumla ya ,mabao 20 katika michezo ya ligi kuu nchini Ureno pamoja na ile ya UCL huku timu ya taifa akifunga mara 17 na kuassist mara 7 katika michezo 33 na tayari wachambuzi mbali mbali akiwemo pia mwanasoka bora wa dunia Cristiano Ronaldo wamemmtaja Andre kama mwokozi mpya wa Ureno.
Cristiano Ronaldo amemtabiria mazuri Andre Silva katika siku zijazo na akisisitiz kwamba hata yeye akiondoka anaamini Ureno itakuwa salama “Kama nikistaafu soka naamini bado Ureno itakuwa salama kwani tuna mshambuliaji bora Andre Silva’ alisema Cristiano Ronaldo.

from Blogger http://ift.tt/2rSnxYW
via IFTTT