Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Suleiman Kova amesema marafiki wengi wa viongozi si marafiki wa kweli bali ni marafiki wa zile nafasi walizonazo.
Kamanda Kova alisema hayo katika uzinduzi wa Chuo Cha Fursa (APEC) kilichopo maeneo ya Ukonga, mwishoni mwa wiki ambapo mkurugenzi wa chuo hicho alimualika kuhudhuria hafla hiyo.
“Mkurugenzi wa APEC, Respicius Timanywa, alikuja ofisini kwangu mwaka 2010 akitaka ushauri na kupata maelekezo kuhusu mtaala wa kufundishia bodaboda, tuliandaa pamoja naye, leo amenikumbuka kanialika katika uzinduzi wa chuo,” alisema Kamanda Kova.
Aliongeza “Ni watu wachache sana wanaoweza kukumbuka, wengi ni marafiki wa kiti chako sio wewe, ukitoka katika kiti ukimpigia simu hapokei na mwingine anaitika kisha anazima kabisa.”
Aidha Kamanda huyo alisema kwa sasa anajishughulisha na kutoa ushauri wa masuala ya maafa, majanga na uokoaji.
from Blogger http://ift.tt/2owCnUD
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2oDXTU1
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nSyXs9
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2oUb7eO
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nXLtrH
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2nXNqEK
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2oy87IA
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2oyo0yo
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2o5W9oP
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2nTGYge
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nGtQdB
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nBjCdC
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2nUIGOE
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2o6Yn7l
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nCaDsz
via IFTTT