Makamu wa Rais wa klabu ya Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kweli suala la taarifa ya nyasi zao bandia kutaka kupigwa mnada, limewashitua sana.
Lakini akawataka mashabiki na wanachama wa Simba kutulia wakati uongozi unapambana katika suala hilo.
“Tokea nyasi hizi zimepita tulifanya juhudi ya kuomba msamaha kwa serikali, unajua nyasi hizi si kwa Simba pekee. Ni kwa kwa jamii yote kwa kuwa tunalenga kuendelea vijana ambao hawatakuwa faida yetu pekee.
“Lakini tumekuwa tukiendelea kupambana kuzitoa, tulishaanza ujenzi wa uwanja na suala la nyasi tu.
“Kuhusiana na taarifa kwamba zinataka kupigwa mnada, kweli linashitua. Unajua kawaida mzigo wako ukikaa bandarini baada ya siku 60, unapewa taarifa ya kupigwa mnada. Tunaendelea kulishughulikia hili,” alisema Kaburu.
Taarifa za Kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart inataka kupiga mnada nyasi bandia za Simba imesambaa kwa kasi leo asubuhi.
Imeelezwa kuwa nyasi hizo zitapigwa mnada leo nyuma ya “The Waterfront Sunset Restaurant and Beach Bar”.
Tazama video Mtoto amvua kofia Papa Francis
from Blogger http://ift.tt/2oe5yM6
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2oBPpvL
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2oCo4d5
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2mT9vW0
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nEpQg4
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nonm2Y
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2oek45Y
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2nB7ISA
via IFTTT