TAARIFA MPYA KUTOKA POLISI KANDA MAALUM DAR ESLSALAAM

·        MAJAMBAZI SUGU SITA WALIOMMUA AFISA WA POLISI ASP ELIBARIKI PALLANGYO WAKATWA. WAPATIKANA NA SILAHA MBILI.


·        WATUHUMIWA WA UGAIDI WAZIDI KUKAMATWA KATIKA OPARESHENI KALI INAYOENDELEA. SABA WASHIKILIWA POLISI KANDA MAALUM. PIA ZIMEKAMATWA BUNDUKI NNE NA RISASI18

jeshi la Polisi kanda maalum ya dar es salaam wamefanikiwa kuwakamatwa majambazi sugu sita walioshiriki katika mauaji ya ASP Elibariki Palangyo huko nyumbani kwake Yombo Makangarawe tarehe 04.08.2015.


waliokamatwa ni: 1) OMARY SALEHE@BONGE MZITO (39) MKazi wa Mtoni mtongani ambaye ni Kiongozi wa kundi hilo

2) SAIDI SAIDI MAZINGE (37) Mkazi wa Tegeta Kibaoni
 3) RASHIDIWATSONB@ DODO(21) MKAZI WA Vingunguti
4)RAMADHANI SALUM@NGUZO 38 mkazi MBAGALLA KIBURUGWA
5) BAKARI SALIM RASHIDI@ MALENDA (38) Mkazi wa Mbagala kizuiani
6) HAMISI HAMISI @ FREEMASON 24 Mkazi wa Mbezi Mwisho
Afisa huyo wa ngazi ya juu katika jeshi la Polisi alikuwa anafanya kazi Mkoani Morogoro katika kikosi Maalum cha kupambana na majambazi aliyekuja nyumbani kwake Dar Es salaam. Alikuja DSM kwa ajili ya kusalimia familia na ndipo alipovamiwa na majambazi usiku wa manane wakati amelala na familia yake.

Aidha mtuhumiwa  namba mmoja alikutwa na silaha bastola aina ya revolver iliyofutwa namba na baada ya mahojiano. aidha mtuhumiwa huyo ambaye kwa sasa ni marehemu kabla ya kufariki alijaribu kuwatoraka askari kwa kukimbia alijeruhiwa na hatimaye alifia njiani wakati akipelekwa hosptalini. Pia inasemekana marehemu alipotezana na familia yake miaka mitani iliyopita akiwa kwenye harakati ya ujambazi. 

Pia bonge mzito alikuwa akitafatwa na Polisi kwa matukio mazito ya ujambazi wa kutumia silaha na mauaji ambaye pia amehusika katika mauaji ya afisa wa Polisi nyumbani kwake usiku wa manane na kumuua mbele ya familia yake ikishuhudia.
Pia mtuhumiwa RASHIDI WATSON@ DODO alikamatwa maeneo ya Vingunguti tarehe 01.10.2015 akiwa na silaha aina ya Shortgun ilikatwa mtutu na kutengenezwa kienyeji ikiwa na risasi nne na betri mbili zilizounganishwa kwa ajili ya kulipua baruti.
Watuhumiwa wengine watano watapelekwa mahakamani baada ya kuperuzi  na kukamilika kwa upelelezi wa shauri hilo.

WATUHUMIWA WA UJAMBAZI WANAOJIHUSISHA WANAOJIHUSISHA NA UGAIDI WAPATAO  SABA WAKAMTWA, SITA KATI YAO NI WAFIMILIA MOJA

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaamkwa kushirikiana na mikoa ya jirani pamoja na vyombo vingine vya dolalimeendelea kufanya oparesheni ya kuwatafuta na kisha kuwakamata wale wote wanaojihusisha na matukio ya kupanga na kuvamia vituo vya Polisi, kuua askari/raia kisha kupora silaha jambo linaloashiriavitendo vya kigaidi.

Oparesheni hiini kali na ya aina yake kwa madhumuni ya kukomesha kabisa vitendo vya uvamizi wa vituo vya Polisi na wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine lazima wakamatwe ili sheria uchukue mkondom wake. Oparesheni hii pia ina lengo la kuwaondolea hofu wananchi dhidi ya vitendo vya kigaidi nchini na kwamba wananchi waendelee kutoa taarifa juu ya watu kama hao ili nchi yetu iendelee kuwa na amani na utulivu.Majina ya watuhumiwa waliokamatwa ni kama ifuatavyo:

1.    SIAD S/O MOHAMED ULATULE @ USO WA SIMBA, Miaka 67, Mkazi wa Mandimkongo, Mkuranga mkoa wa Pwani.

2.   RAMADHANI S/O ALLY NGANDE, Miaka 29, Dereva wa Bodaboda, Mkazi wa Kongowe.
3.   HAMIS S/O MOHAMED SALUM SIMBA ULATULE, Miaka 51, Mkulima, Mkazi wa Mamdimkongo, Mkuranga, Pwani.

4.   ALLY S/O MOHAMED SALUM SIMBA ULATULE, Miaka 65, Mkulima, Mkazi wa Mamdimkongo, MKuranga, Pwani.

5.   NASSORO S/O SELEMAN ULATULE, Miaka 40, Mkulima, Mkazi wa Mamdimkongo, Mkuranga, Pwani.
6.   SELEMAN S/O ABDALLAH SALUM ULATULE, Miaka 83, Mkulima, Mkazi wa Mamdimkongo, MKuranga, Pwani.

7.   SAID S/O ABDULLAH CHAMBETA @ Mzee wa Fasta, Miaka 40, Mfanyabiashara wa Mitumba, Mkazi wa Yombo Makangarawe.Mtuhumiwa namba 1,3,4 na 5 ni wa familia moja inayojihusisha na vitendo vya ujambazi pamoja na  vya kigaidi.

Tunawashukuru sana watanzania wazalendo na wenye mapenzi mema na nchi yao kwa kutoa ushirikiano wa hali na mali ambao umesaidia kupata mafanikio yote haya.Tunawaomba waendelee kulisaidia Jeshi la Polisi kwa kuendelea kutoa taarifa ili oparesheni hii iwe yenye ufanisi zaidi.

KUKAMATWA KWA BUNDUKI SMG MOJA NA SHORTGUN MBILI, BASTOLA MOJA PAMOJA NA RISASI 14.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi linamshikilia mtuhumiwa MUSSA S/O MALAKI AKUTI, Miaka 30, fundi wa magari, Mkazi wa Mbagala Charambe kwa kukutwa na bunduki aina ya “Chinese 56 SMG” yenye namba 563845189 ikiwa na magazine moja na risasi 14. Mtuhumiwa huyu alikamatwa tarehe 28/09/2015 maeneo ya Mbagala Sabasaba, Temeke jijini Dar es Salaam baada ya Polisi kupokea taarifa kutoka kwa raia wema.