Mfanyakazi Takukuru mbaroni kujiandikisha mara mbili

JESHI la Polisi mkoani njombe linawashikilia watu 15 kwa tuhuma za kujiandikisha mara mbili katika daftari la kudumu la mpigakura kwa mfumo wa Biometric Votar Regstrestion (BVR) akiwemo afisa wa tume ya kupambana na Rushwa Tanzania Takukuru wa wilayani Ludewa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Wilbroad Mtafungwa akizungumza na waandishi Agosti 2015Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa semina kwa Askari Police, Magereza na Mgamo wa wilaya ya Njombe kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, Wilbroad Mtafungwa (Pichani) alisema kuwa jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu 15 walio jiandikisha mara mbili mkoani huo na kuwa linaendelea na msako wa watu wengine ambao walijiandikisha marambili.

Alisema kuwa kati ya watu hao kuna baadhi yao wamepandishwa mahakamani katika mahakama za wilaya zao na kuwa mmoja kati ya walio pandishwa mahakamani amekubali kosa na kulipa faini ya shilingi laki moja (100,000).

Alimtaja mshitakiwa aliye kili kutenda kosa hiyo kuwa ni Awatich Sanga mkazi wa Mfumbi Makete, alifikishwa mahakanani na kukubari kosa na kutozwa faini ya shilingi laki moja,(100,000) wengine bado kufikishwa mahakanani kutokana na upelelezi kuwa haujakamilika.

Alisema kuwa kati ya walio kamatwa kunamfanyakazi wa Takukuru ambaye naye amekamatwa kwa tuhuma za kujiandikisha marambili ambaye alitambulika kwa jina la Abdul Badenga mkazi wa Manda Ludewa na kuwa atafikisha mahhakamani upelelezi utakapo kamilika.

Mtafungwa aliwataja watu wengine walio kamatwa kwa tuhuma hizo kuwa ni Esta Mgimba, John Mlingo, wote wakazi wa Ramadhani Walda Mahegema mkazi wa Chaugingi, Bonfasi Mwalongo, Christina Sange, Adgia Ngwazi, Esta Mhando, Samson  Mgaya, wakazi wa wilaya ya Wangingombe, Helena mpanmgala Saulo Haule, Maria Chaula Jonasan Haule na kuwa huyu amefikishwa mahakanani.

Aliongeza kuwa katika wilaya ya Makambako alikamatwa mtu mmoja Jeska Chenana, alisem akuwa wengine wanaedelea kutafuwa ili kujibu mashitaka yanayo wakabili hasa ya kujiandikisha marambili.


Hata hivyo walio baki kufikishwa mahakamani bado upelelezi wa jeshi hilo unaendelea ili kujibu tuhuma zinazo wakabili watu hao.