Waumini nchini waonywa wanao toa pesa kipindi hiki

WAUMINI mbalimbali hapa nchini wametakiwa kutumia vizuri kipindi hiki cha uchaguzi kwani wakifanya vibaya sasa watapata shida miaka mitano, na kuepuka wanao wapa pesa na kuonywa kuwa hizo sio pesa ni rushwa.

Wito huo umetolewa na mchungaji wa kanisa la Pendekosti Holiness Mission la mkoa wa Njombe Mch. Joseph Mtweve akiwa katiba ibada ya Jumapili iliyopita.

Alisema kuwa katika wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali wameenda timu ya kuliombea taifa dhidi ya machafuko na viashiria mabilmbali vya machafuko na upotevu wa amani.

Alisema kuwa waumini na Watanzania kwa ujumla mwaka huu wanatakiwa kuhakikisha wanaepuka kupewa poesa na watu wanao gombea kwa kuwa wanawapa pesa na misaada hiyo sio misaada ni Rushwa kwa kuwa kipindi chote mtu huyo hakuona umuhimu wa kusaidia jamii lakini kipindi cha uchaguzi ndio wanaona ndio mwafaka wa kutoa misaada.

Alisema kuwa: “Waumini kipindi hiki tulicho nacho ni kigumu kufanya maamuzi ya miaka mitano ijayo kama tukifanya vizuri kipindi hiki basi kwa miaka mitano tutakiwa vizuri na tukifanya vibaya ni kwa miaka mitano ndio tutaondoa ubaya huu,” alisema Mtweve.

Alisema kuwa haiwezekani kwa mkristo kuwa na makundi wakati huu mkristo kazi yake ni kuombea ili Mungu atoe kiongozi bora kama wakristo wakiwa na makundi hapo watachagua kiongozi kwa utashi wao.
Wakati huo huo amewataka waumini kote nchini kuhakikisha kuwa wanaenda kupiga kura siku ya kupiga kura kwa kuwa bila kufanya hivyo watachaguliwa kiongozi wasiye mtaka.

“Siku ya uchaguzi wote wenyesifa mkapige kura haitawezekana kuwaachia watu wengine wakawapigia kura mkachague kiongozi ambaye anafaa na hatoi toi rushwa ili kuwa na kiongozi anayefaa,” alisema Mtweve.

Alisema wakati kumebakiwa na miezi michache kumekuwa na ushawishi badili kwa wanao wania uongozi wananchi wajiepushe nao hao hawana dhamira ya kweli ya kuongeza wananchi.

Alisema kuwa ukiona mtu anatoa pesa huyo anaenda kuchukua uongozi kwa manufaa yake mwenyewe ndio maana anaingia gharama za kutoa pesa ili apate.