Matokeo kwa majimbo yote ya mkoa wa Njombe yapo hapa


MATOKEO katika jimbo la Makete Mkoani Njombe mbunge Binilith Mahenge ameongeza katika kura za maoni zilizo fanyika juzi huku changamoto ya miundombinu ikileta utata wa kutoa matokeo mapema.

Katibu wa CCM mkoa wa Njombe Hosea Mpagike Akizungumza na Elimtaa alisema kuwa kutikana na changamoto za miundombinu ya jimbo la Makete matokeo hayo jamemfikia usiku wa kuamukia jumatatu.

Alisema Katika jimbo hilo kulikuwa na wagombea watano walliokuwa waking’ang’a kuchaguliwa na wananchi kuwakilicha chama chao katika uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu mbunge wa jimbo hilo Binilith Mahenge alipata kura 8534 Norman Sigala kura 8211, Bonic Muhami 500, Fabianus Mkingwa kura 466 na Lufunyo Rafael 226.

Alisema matokeo hayo kutoka jumamosi jioni yalikuwa yakihesabiwa na kukusanywa kwa tabu kutokana na Jografia ya maeneo ya wilaya hiyo.

“Kunamaeneo ambayo hayafikiki na kuwasilisha matokeo kwa njia ya simu wanawasiwasi hivyo imewalazimu kupelkeka karatasi za matokeo wazizo saini mawakala mpaka ofisi za wilaya,” alisema Mpagike.

Alisema kulingana na matokeo hayo Mahenge mbunge wa sasa ndio ata ongoza katika majina yatakayo pelekwa katika kamati kuu ya CCM na itarudisha jina tena kwaajili ya kuingizwa kwa wananchi kupigiwa kura.

Kwa matokeo hayo Wabunge wote walio kuwa madarakani wameshinda kwa kishindo huku majimbo yaliyo gombewa na Wabunge waliokuwa wanatetea nafasi zao ni manne ambayo Wabunge hao wameshindwa kwa kishindo.

Jimbo la Makambako lilikuwa chini ya Deo  Sanga kura 7643 huku mgombea mwenzake akiwa hajafika hata nusu ya kura zake, Alimwimike Sahi 499, na walikuwa wawili katika jimbo hilo,  jimbo la Ludewa kulikuwa na Deo Filikunjombe ameshinda kwa kura 18290 huku akiwagaragaza wagombea wenzake kwa kura nyingi  ambao walikuwa watatu katika jimbo hili na hata nusu hawajafikia.

Katika jimbo lingine ni la Njombe Magharibi lilikuwa na chini ya Greison Lwenge ambaye alipata kura 13715 huku aliye mfuatia akijaribu kumkaribia na alikuwa mbunge wa jimbo hilo kabla yake Thomas Nyimbo kura 2296 na mbunge mstaafu mwingine Yono Kevela 1900 na wengine wengine tisa wakitupiwa mbali , Petro John, 467 Richard Magenga  417Abraham Chaula 382 Danford Mpumilwa 332, Hoseana Bumogero 322.

Majimbo mawili ya Njombe yanawagombea ubunge wapya ambayo ni jimbo la Lupembe ambalo mshindi ni Joram Hongoli aliyepata kura 2233 huku akiwatupa mbali wenzake walio kuwa nane Jeston Kaduma, 1912 Oska Msigwa, 1656 Emmanuel Nyagawa, 1083 Avike Kyenga, 836 Lenda Hongoli, 471 Leila Malekela, 365 Osmondi Malekela 103. 

Aidha katika jimbo alilokuwa spika wa bunge la Tanzania Anna Makinda limepata mbunge mpya Edward Mwalongo kwa kupata kura 3870 ambapo saba walio mfuatia walipambana na kuzidiwa kwa kura zaidi ya 1000 aliye mfufuata kupata kura 2158 Lomanus Maemba Dioniol Msemwa 1676, Alnod Mtewele, 186, Alfred Luvanda 978, Laulian Mwaijinga 86, Hassan Mkwawa 152, Vitalis Konga 76.