WATOTO SHAKANI KUPATA HUDUMA KAMA UNICEF WAKIJITOA


IMEDAIWA kuwa huduma za ulinzi wa mtoto Mkoani Njombe zikafikia ukomo baada ya wafadhili kujitoa, kutokana na fedha zilizopo kwa asilimia kubwa kutoka kwa wafadhili.

Akizungumza katika kikao cha mw2aka cha tathimini ya ulinzi wa mtoto mkoa wa Njombe, afisa Maendeleo ya jamii halmashauri ya wilaya ya Njombe Justoni Chaula alisema kuwa kuna wasiwasi wa watoto kuto pata huduma ya ulinzi kutokana na kuto kuwapo kwa fedha za kutosha kutoka ndani ya nchi kwaajili ya  ulinzi wa watoto.

Alisema kuwa wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali na kupambana na wanao wanyanyasa watoto kutokana na vijiji vingi kuto kuwa na polisi katika ofisi za kata na kutumia askali mgambo ambao wengi wao ni wazee.

Alisema kuwa licha ya kuwa na mgambo hao wazee kumekuwa na kasumba ya watu wanao wanyanyasa watoto kutoroka katika mahali walipo hifadhiwa baada ya kukamatwa.

Alisema kuwa licha ya kuwa na uhaba wa mahali pa kuwahifadhi wahalifu dhidi ya watoto kumekuwa na changamoto za migamo hao waliopewa mafunzo ya kuwadhibiti na kutambua uharifu dhidi ya watoto wamekuwa dhaifu kutokana na umri wao na kushindwa kuwadhibiti waharifu.

Alisema ofisi yake inayo fadhiliwa na shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikia watoto (Unicef) katika mradi wa ulizi wa watoto wamekuwa wakiwasaidia kufika vijijini kutoa elimu juu ya ukatili na kuanzishwa timu za ulinzi wa mtoto huku fedha kutoka serikalini kuto kuwepo katika shuguli hizo.

Kutokana na kuto kuwapo kwa fedha za serikali anawasiwasi baada ya kujitoa shirika hilo kuna uwezekano mkubwa wa kukwama kwa huduma hiyo.

Hivyo aliiomba serikali kuhakikisha kuwa kunakuwepo na vituo vya polisi katika kata za mali na mijini ili kusaidia ulizi wa jamii na watoto.

Aidha Chaula alitaka tume ya ajira kuhakikisha kuwa inaajili wafanyakazi wengi wa Maendeleo ya jamii ili kuisaidia jamii ya vijijini hasa kulinda mtoto asipatwe na manyanyaso .

Akifungua mkutano huo kaimu katibu tawara mkoa wa Njombe Lameck Noah alisema kuwa watoto wanahitaji upendo wa hali ya juu ili kuepusha jamii yenye ukatili na visasi.

Alisema; “Mtoto anaye ishi kwa manyanyaso akikuwa anakuja kuwa mtu hatari sana kwakuwa anaharibika kisaikolojia na kuwa na asili ya ukatili mtupu lakini akilelewa katika malezi bora anakuwa na upendo wakati wate atakapo kuwa mtu mzima,” alisema Noah.