![](http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/07/23/150723124109_usajili_wa_kielektroniki_tanzania_umeanza_624x351_bbc_nocredit.jpg)
Leo imeingia siku ya pili kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam kujiandikisha katika daftari la kupiga kura kwa kutumia mfumo wa kieletroniki maarufu kama BVR.
![](http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2015/07/23/150723123955_usajili_wa_kielektroniki_tanzania_umeanza_624x351_bbc_nocredit.jpg)
Katika zoezi hili ambalo linatarajiwa kudumu kwa siku kumi, tume ya uchaguzi ya taifa inatarajia kusajili wakazi wapatao milioni tano ambao wana sifa ya kupiga kura.
![](http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2015/07/23/150723124032_usajili_wa_kielektroniki_tanzania_umeanza_624x351_bbc_nocredit.jpg)
Hata hivyo, wakati zoezi hilo likiendelea, tayari linaonekana kuwa kero miongoni mwa wakazi.
![](http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2015/07/23/150723123843_usajili_wa_kielektroniki_tanzania_umeanza_624x351_bbc_nocredit.jpg)
Katika baadhi ya vituo ambao inaarifiwa kuwepo kwa ucheleweshwaji huku katika maeneo mengine kukiwa na mashine chache za uandikishaji.
![](http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2015/07/23/150723123917_usajili_wa_kielektroniki_tanzania_umeanza_624x351_bbc_nocredit.jpg)
Je umejiandikisha kupiga kura katika mfumo huo mpya wa kielektroniki?
Tusimulie yaliyokusibu