Njombe maduka yafungwa

WAKAZI kutoka sehemu Mbalimbali za mkoa  wa Njombe wamewalalamikia wafanyabiashara waliofunga maduka yao kwa siku nzima ya jana kwa kuwa hawakuwapa taarifa ya kufungwa kwa maduka wakati wametumia gharama kufuatia bidhaa.

Baadhi ya wafanyabiashara kutoka wilaya ya Mkoa wa Njombe ambao walikuja mjini hapa kwaajili ya kujumua bidhaa wamelalamikia kitendo cha kufungwa kwa maduka bila ya wao kuwa na taarifa.

Nikolas Mahundi mkazi wa wilayani Ludewa alisema kuwa ametoka wilayani kwake akitegemea kukuta maduka yakiwa wazi na kununua bidhaa kwa ajili ya duka lake lakini alicho kutatana nacho ni makufuri katika maduka ambayo amekuwa akinunua bidhaa za jumla.

Alisema kuwa wafanyabiashara ni bora wakawa wanatoa taarifa ili wasitumie gharama kuja mjini na kuwa sasa wamewaongizea gharama kwa kuwa wanahitajika kulala kwa kuwa hakuna gari inayoenda wilayani huko ikifika majira ya jioni.

Alisema kuwa angekuwa na taarifa asinge kuja mjini na kuwa hiyo ni adhabu kwao licha ya kuwa wamefunga kwa malengo mazuri.
“Kufungwa kwa maduka tuwe tunapata taarifa na sisi wenzenu ili tusije tunapo kuja huku na kukuta madrka yamefungwa mtatutesa wenzenu jamani,” alisema Mahundi

Naye Jonasan Sanga mkazi wa wilayani Makete alisema kuwa kufungwa kwa maduka kumemuongezea gharama ya kulala mjini Njombe wakati alitakiwa kufika na kujumua mziko kisha kurudi.

Alisema kuwa wafanyabiashara ni bora kama wanataka kufunga maduka siku moja kabla wakiwa wanatangaza ili wanao toka wilayani wasije mjini.

Wafanyabiashara Mkoani Njombe wamefunga maduka kwa lengo la kusikiliza kesi ya Mfanyabiashara mwenzao Jonson Minja ambaye kesi yake inasikilizwa tena jana Mkoani Dodoma na kuwa wafanyabiashara wamekuwa wakifunga maduka kila siku ya kusikiliza kesi hiyo.

Kwa upande wa viongozi wa wafanyabiashara walisema watalizungunzia suala la kufunga kwa maduka baada ya kufanya mawasiliano na kuwa watawajulisha wanahabari.



Picha na Elimtaa Photographer