Mgogoro Wamalizika wa Rea na WanaRamadhan, Umeme wapita

MGOGORO uliokuwepo baina ya wananchi wa mtaa wa Ranadhani halmashauri ya Njombe na mkandalasi wa umeme wa Umeme vijijini (Rea), umemalizika ambapo wananchi walikuwa wanakataa kupitishwa umeme katika viwanja vyao na sehemu wanazotaka kujenga.

Akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la Ramadhani ulikukuw amgogoro baada ya kuonyesha eneo la kupitisha umeme unaoenda vijijini, Meneja wa Tanesco mkoa wa Njombe, Eng Andrew Kichiwa,  alisema kuwa wananchi walicho kuwa wakipingana na Rea ni kupitishwa nguzo hizo katika makazi yao ambapo msanifu mradi hakuzungumza na wananchi wakati wa kuweka mradi huo.

Alisema mgogoro huo umeisha baada ya wananchi kuonyesha maeneo ambayo mradi huo unatakiwa kupita tofauti na ambapo ulitakiwa kupita awali maeneo ambayo ni makazi yao na kuonyesha maeneo ambayo ni barabara za mitaa na kupitisha umeme huo.

“Katika eneo hili wananchi walikuwa wanakataa kupita umeme kutokana na msanifu wa mradi alipitisha umeme katika makazi yao na katika hifadhi ya barabara kulikuwa nyumba za watu ambao wanatakiwa kulipwa fidia na bado hawajalipwa na haijulikani watalipwa lini,” alisema .
Meneja aliongeza: “Mradi unamdawake wa kuisha umeme unahitajika kupitishwa hivyo mgogoro umemalizwa kwa kuzungumza na wananchi na kuonyesha sehemu ya kupita umeme,” aliongeza. 

Kilicho leta mgogoro baina na wananchi kinadaiwa ni ushirikishwaji wa wananchi wakati wa kuweka mradi huo ambapo wananchi hawakutaka nguzo za umeme huo kusimikwa katika maeneo ambayo tayali wanaplani za kujenga.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Ramadhani, Bathomeo Kyando alisema kuwa mgogoro huo umetokana na kuto washirikisha wananchi wakati wa uwekaji wa nguzo zizo na kuwa mgogoro huo hautajitokeza tena kwa kuwa wananchi wenyewe wameonyesha eneo la kupita mradi huo.

“Tatizo hili lilijitokeza kutokana na ushirikishwaji wa wananchi haukuwepo ndio maana kumekuw ana mgogoro na mkandalasi kupata kazi ya kuweka na kutoa nguzo katika eneo hili lakini baada ya mazungumzo na wananchi na wameonyesha maeneo ya kupita mradi hakutakuwa na mgogoro tena mradi utapita bila kuw ana wasiwasi,” alisema Kyando.

Kwa upande wa wananchi walisema kuwa walishangaa kuona nguzo zinawekwa katika maeneo yao ambayo wanatarajia kujenga baada ya kufukuzwa na wakala wa barabara Tanzania (Tanroad) baada ya kulipwa fidia.


Walisema kuwa kwa maeneo ambayo wameonyesha umeme upiti hawana pingamizi na umeme utapita bira ya kuwapo kwa matatizo yoyote na wao wanafurahi kuona wenzao wanapata umeme lakini kwa kupitisha katika makazi yao hawakufurahia.