WATOTO MAPACHA WALIOUNGANA VIFUA NA MATUMBO WAZALIWA MKOANI MARA

Mwanamke mmoja mkazi wa kata ya Buhare katika manispaa ya Musoma mkoani Mara Bi.Helena Paulo mwenye umri wa  miaka 20 amejifungua watoto wawili mapacha ambao wameungana katika eneo la kifua  hadi tumboni tukio  ambalo limevuta mamia ya wananchi ambao wamefika katika Hospitali ya rufaa  mkoa wa Mara mjini Musoma  kwa lengo  la kutaka  kushuhudia tukio  hilo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika  wodi ya wazazi katika Hospitali hiyo  ya  rufaa ya  mkoa  wa mara mjini ,Musoma,muuguzi wa zamu Bi. Naabu Geraruma,amesema kuwa  mwanamke huyo  amefanikwa kujifungua usiku wa  saa saba kuamkia leo Jumatatu   kwa  njia ya operesheni watoto hao wawili  wenye jinsi ya kike huku wakiwa na uzito wa kilo
4.6
Hata hivyo muuguzi huyo wa zamu amesema tukio hilo ni la kwanza  kutokea katika Hospitali ya mkoa wa Mara na kwamba hali za  mwanamke huyo na watoto zinaendelea  vema na taratibu za  kumpeleka hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza   zimekamika.
Hata hivyo mkurugenzi wa utawala na rasmali watu wa  hospitali ya rufaa ya Bugando Bi.Leah Kagine amesema tayari  mwanamke  huyo   na watoto  wamefikishwa  katika hospitali ya  rufaa kwa ajili ya matibabu na uchunguzi zaidi.
via>>ITV