Askali Polisi watatu wafukuzwa


  • Waliliuka miiko ya kazi 
RPC NJOMBE
  RPC NJOMBE Fulgence Ngonyani
Jeshi la polisi mkoani Njombe limeamua kuchukua uamuzi mgumu wa kuwafukuza kazi askari polisi wake watatu kwa makosa mbalimbali waliyoyafanya ikiwemo vitendo vibaya kinyume na sheria za jeshi hilo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa mtandao huu na Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe SACP Fulgence Ngonyani (pichani) askari hao waliofukuzwa kazi ni EX.G. 3172 PC Ramadhani Iddi Saidi, EX.G. 9693 PC Emmanuel Morson Lyimo pamoja na EX.G. PC Miraji Jumanne Mtea.
Kamanda Ngonyani amesema Jeshi la polisi limeamua kutoa adhabu hiyo kali kutokana na vitendo mbalimbali vya utovu wa nidhamu walivyovifanya ikiwemo tukio la hivi karibuni la kupigana hadharani Septemba 2 mwaka huu Mjini Njombe.
Amesema wanategemea adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa askari wengine wenye tabia kama hiyo kwani jeshi halitawavumilia askari wake ambao wanakwenda kinyume cha sheria.
Katika hatua nyingine Kamanda Ngonyani amewataka wananchi kuwa makini na askari hao waliofukuzwa kazi huku akisisitiza wananchi kutambua kuwa askari hao si watumishi tena kuanzia Oktoba 24, mwaka huu.