SITTA: MKOME MNAOTAKA KUANZISHA CHAMA KINGINE

WALIMU wanaotaka kuanzisha chama chao tofauti na chama cha walimu Tanzania (CWT) watakiwa kutokianzisha chama hicho, badala yake wapendekeza mapungufu ambayo yanayohitajika kuondolewa katika chama cha walimu ili kuto tokea mgawanyiko.
 
Akizungumza na viongozi wa wanawake wa chama cha walimu Tanzania mkoa wa Dodoma (CWT) aliyekuwa waziri wa elimu mbunge wa viti maalum Margret Sitta (CCM) jana alisema kuwa walimu wanatakiwa kuboresha chama ili kiwe na nguvu ya kudai haki zao  na siyo kuwa na mitazamo ya kuanzisha chama kingine.

Mbunge huyo  alisikitishwa na baadhi ya kauli za walimu ambao wanaotaka kuanzishwa kwa chama kingine, alisema kitendo hicho ni uchu wa madaraka wa kutokana na kukiacha chama chao cha  CWT ambacho kwa sasa kinaendelea kutetea wanataaluma ya ualimu.

Sitta alisema kuwa kuanzishwa kwa chama kingine cha waalimu hapa nchini kutapunguza nguvu waliyo nayo kutoka na na chama hicho.

“Nilisikitishwa siku moja tuko bungeni walikuja watu wanao taka kuanzisha chama kingine cha waalimu, hivi tutakuwa waalimu mtakuwa na mgawanyiko sana na mtashindwa kuwa na umoja ambao mnao hivi sasa kwa kuwa kila chama kitakuwa na madai yake,” alisema Sitta.

Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa chama kingine cha waalimu waalimu wa takuwa wameanza kugawanyika kwa sabau kila chama kitakuw ana madai yake kutoka na chama kinavyo jisikia tofauti na sasa kumekuwa na sauti moja ya waalimu.

Alisema wanaotaka kuanzisha chama kingine wanatakiwa  kuwa karibu na  chama ili kujua nini chama hicho kina mapungufu gani ili kufanya marekebisho na kukiwezesha kuwa na maendeleo kwa ajili ya walimu.

Aliongeza kuwa mgawanyiko hautawanufaisha bali utazorotesha katika kudai mahitaji yenu  kutokana na jitihada zilizopo za ambazo zimefanya  chma kupata  mafanikio ya kuwasaidia waalimu wengi kutatua shida zao na kujenga majengo  yao kila mkoa hapa nchini kutoka na pesa zinazo changwa na wanachama kila mwezi.

Alisema chama kwa sasa kinaweza kufanya maamuzi yake kutoka na kuwa na vitega uchumi vyake na kutatua kwa urahisi matatizo wanayo kabiliana nayo waalimu kote nchini.