MBOWE: SUALA LA MAJI LIWE KAMA SHERIA KWA SERIKALI ILIYO MADARAKANI


MWENYEKITI wa chama cha Demokrasia na Maendeleo chadema Freeman Mbowe amewataka wakazi wa Mbeya kutuma maoni ya katika na kuwekea mkazo suala la maji kuwemo katika katiba mpya.

Alisema kuwa katiba mpya iweke suala la kuwapatia maji lewemo katika katika na iwe ni lazima kwa kiongozi atakaye kuwa madarakani kuwapatia maji wananchi.

Aliyasema hayo juzi katika mkutano wa hadhala mkoani Mbeya na kuwataka wakazi hao kuliweka suala la maji kuwa ni haki ya msingi kwa kila mwananchi.

Alisema kuwa kiongozi yeyote atakaye ingia madarakani kuhakikisha wananchi wote wanapata maji na itakuwa ni kama sheria likiwekwa katika katiba.

“Ni aibu kwa nchi kama hii iliyo zungukwa na maji kila kona lakini kuna wananchi hawana maji na katika Afrika nzima nchi pekee ya Kongo ina maji kwa wananchi wote na kwa Tanzania amboyo emezungukwa na maziwa na mito kuna wananchi hawana maji” alisema Mbowe.

Aliongeza “Hata kama Chadema ikiwa madarakani au CCM ama chama chochote kikishika dora lazima kiweke mbele suala la maji kwa kila mwananchi”

Alisema kuwa wananchi bado wananafasi ya kutoa maoni ya kuchangia katika maoni ya katiba kupitia chama chao kwa kutuma maoni kabla ya kufika Augosti 31 ambapo itakuwa mwisho wa kupokea maoni kwa tume ya katiba mpya.

Aliongeza kuwa Chadema inazunguka nchi nzima kukusanya maoni ya wananchi ma kupeleka maoni hayo katika tume ya katiba.