MBEYA: WANATUNDUMA ACHANENI NA MAANDAMANO

JESHI la Polisi Mkoani Mbeya limewataka wakazi wa Tunduma kuacha kujiingiza katika maandamano yasiyo na tija kufuatia uvumi ulionezwa kuwa barabara kati ya Mwaka na Tunduma yenye umbali wa kilometa mbili ahaitojengwa.
Katika taarifa yao mapema leo asubuhi kwa vyombo vya habari imesema kuwa barabara hiyo haipo chini ya mamalaka ya mji mdogo wa Tunduma bali ipo chini ya TANROADS hivyo kwenda kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya mji huo ni makosa.
Hayo yanajiri kufutia uvumi kuwa leo kutakuwa na maandamano kwa wakazi wa Tunduma na vitongoji vyake kupinga hatua hiyo ya kutoijenga barabara ya Mwaka hadi Tunduma hali ambayo ingeendeleza ajali katika eneo hilo.
Hata hivyo kuna taarifa zisizo rasmi kwamba Diwani wa eneo hilo kuwa yeye ndiye mwanzilishi wa vuguvugu la maandamano hayo na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.