SWAYA WAIOMBA SERIKALI MAJI



BAADHI ya wakazi wa kata ya Swaya Halmashauri ya Mbeya Mkoani hapa wameiomba Serikali kuwafanyia fufumbuzi wa tatizo la maji katika katayao ambalo limekuwa kelo katika Kata yao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Elimtaa wamesema wamekuwa wakipata shidi ya kufuata maji kwa zaidi ya kilomita mbili kutoka katika makazi yao wakati wa kipindi cha kiangazi licha ya mradi wa maji unaotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni chanzo chake kuwa katika kata hiyo.

Afisa mtendaji wa kata hiyo Bw. Suto Julius amesema kuwa wananchi wa kata hiyo hasa wanawake wamekuwa wakifuata maji kwa umbali wa zaidi ya kulomita mbili kotoka katika kata hiyo.

Amesema wanawake wamekuwa wakitumia mda mwingi wa kufanyamaendeleo katika harakati za kutafuta maji.

Mmoja wa weakazi wa kata hiyo Bi. Sabet Ntokani amesema kuwa huwawanapata shida sana kwanyakazi za kiangazi kwa kufuata maji kwa umbali mrefu kutoka katika makazi yao na kuteka maji yaliyo tuama hayo katika mto Swaya.