Showing posts with label Hatma ya kesi ya Kenyatta. Show all posts
Showing posts with label Hatma ya kesi ya Kenyatta. Show all posts
Rais Kenyatta tayari kwenda ICC

Rais Kenyatta tayari kwenda ICC

  • Amkabidhi urais makamu wake.
  • Aenda kwa mguu ikulu kutoka ukumbi wa bunge, Aenda Icc kama raia wa Kenya na sio Rais

A
Rais Kenyatta amesisitiza hana hatia na wala hana hofu kuwa mahakama itaamua vinginevyo
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema yuko radhi kwenda katika mahakama ya kimataifa ya ICC kwa kikao maalum kuhusu kesi inayomkabili.
Akiwahutubia wabunge mjini Nairobi,aliwaambia kuwa yuko tayarti kuhudhuria kikao maalum alichotakiwa kuhudhuria mjini Hague bila wasiwasi wowote.
Kenyatta alitakiwa na majaji wa mahakama hiyo kufika ICC tarehe 8 mwezi huu kufafanua madai kuwa serikali yake imekataa kushirikiana na mahakama hiyo hasa upande wa mashitaka kwa kukataa kuipatia ushahidi unaohitajika katika kesi inayomkabili.
Rais Kenyatta anasema anajiamini na kwamba anajua hana hatia katika tuhuma zinazomkabili
Anakabiliwa na tuhuma za kupanga ghasia za kikabila zilizokumba nchi hiyo baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/2008.
Aliarifu bunge kuwa anajiamini mwenyewe kiasi cha kuwa tayari kufika mbele ya ICC na kwamba anajua hana hatia katika kesi inayomkabili.
Alisema Kenya ni nchi huru na kwamba haitawahi kuwa chini ya mamlaka nyingine yoyote.
Kenyatta na naibu Rais William Ruto ambaye pia anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC
Takriban wabunge miamoja wanajiandaa kuambatana na Kenyatta Hague katika ishara yao ya kumuunga mkono.
Uhuru amemkabidhi mamlaka kwa muda naibu wake William Ruto hadi atakaporejea.
Raila Odinga atandikwa bakora

Raila Odinga atandikwa bakora

Mzee Mdzombo anasemekana kutokuwa timamu kiakili
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amemsamehe mzee aliyempiga bakora katika mkutano wa hadhara wa kisiasa katika jimbo la Kwale Pwani ya Kenya,
Mwanamume huyo, Lengo Mdzombo, anayefanya kibarua katika shamba moja Kwale, alikamatwa Jumanne na kufikishwa mahakamani.
Alishitakiwa kwa kosa la kumshambulia kiongozi huyo pamoja na gavana wa Kwale.
Hali ya taharuki ilitanda katika mkutano wa hadhara Jumatatu wiki hii baada ya Mdzombo kwenda ukumbini na kuanza kumtandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Raila alikuwa ameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga
Mzee huyo alimpiga bakora Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanamume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wanasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu.
Hatma ya kesi ya Kenyatta na Ruto kujulikana leo

Hatma ya kesi ya Kenyatta na Ruto kujulikana leo


Umoja wa Afrika unalitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo kupiga kura kuahirisha kwa mwaka mmoja kesi ya uhalifu wa kibinaadamu dhidi ya viongozi wa Kenya katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya ICC.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na makamu wake William Ruto
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na makamu wake William Ruto
Wanadiplomasia wanasema kuwa rasimu ya azimio hilo linalotaka kuahirishwa kwa kesi inayomkabili Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na makamu wake, William Ruto, linaonekana kushindwa kutokana na kutoungwa mkono kwa kiasi kikubwa. Ni wanachama saba tu kati ya 15 wa baraza hilo, ndiyo wanaliunga mkono azimio hilo.
Ili liweze kupitishwa, azimio hilo linahitaji kupigiwa kura na wanachama tisa, lakini hata hivyo, linaweza kupingwa kwa kupigiwa kura ya turufu na mataifa kama vile Uingereza na Ufaransa, yanayoiunga mkono kwa kiasi kikubwa Mahakama ya ICC, iliyoko The Hague.
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, Fatou Bensouda
 
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, Fatou Bensouda
Marekani bado haijajiunga na mahakama hiyo kupitia mkataba wa Roma, lakini inaunga mkono malengo yake.
Umoja wa Afrika unasema kwamba kuahirishwa kwa kesi hiyo, kutaipa Kenya muda wa kuimarisha usalama wake katika kukabiliana na vitendo vya kigaidi, baada ya mashambulizi ya kigaidi ya mwezi Septemba mwaka huu.
Shinikizo lilitokana na shambulizi la kigaidi
Shinikizo la kuahirishwa kwa kesi hiyo limeongezeka baada ya kutokea mashambulizi hayo ya kigaidi yaliyosababisha mauaji ya watu 67 na wengine kadhaa kujeruhiwa. Hata hivyo, wanadiplomasia wa mataifa ya Magharibi na wanaharakati wanaiona hatua hiyo kama kampeni ya kisiasa.
Mahakama ya ICC imewafungulia Kenyatta na Ruto mashtaka ya uhalifu dhidi ya ubinaadamu kwa kuhusika kwao na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, ambazo zilisababisha zaidi ya watu 1,000 kuuawa. Kenyatta anashtakiwa kwa ubakaji na vitendo vingine vya ukatili vilivyofanywa na kundi la kihalifu linalojulikana kama Mungiki, ambalo linadaiwa lilikuwa chini yake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon
Kenyatta aliyechaguliwa kuwa rais wa Kenya mwanzoni mwa mwaka huu, amesisitiza kuwa hana hatia, kama ilivyokuwa kwa makamu wake, William Ruto, ambaye kesi yake tayari imeanza kusikilizwa.
Ama kwa upande mwingine, kura ya maoni iliyoendeshwa nchini Kenya, imeonyesha kuwa asilimia 67 ya Wakenya wanataka Rais Kenyatta ahudhurie kesi dhidi yake huko ICC, ili akajibu shutuma zinazomkabili. Utafiti huo uliofanywa na shirika la Ipsos Synovate, unaonyesha kuwa asilimia hiyo ya raia 2,060 wa Kenya walioulizwa, waliona ni bora Rais Uhuru aende ICC kujibu kesi dhidi yake.
habari na Dw.DE

Kategori

Kategori