HISTORIA
YA KALE HADI FREEMASONS
KARATASI za kale za Wasumeria
zinaeleza kwamba ANNUNAKI waliokuja
na vyombo vieleavyo angani vyenye maumbile kama ya UNGO. Walikuwa ni kabila la MIJUSI au zaidi ya reptilia.
Wayahudi, wamelitaja hilo kama NEFILIM kwa maana ya watoto wa miungu
au AWWIM; neon linalomaanisha viumbe
watambaao kwa tumbo. Wafalme wa Misri mara zote wamekuwa wakihusishwa na NYOKA na REPTILIA.
Mtafiti mmoja wa Kimarekani DAVID SIELAFF anasisitiza kwamba NEFILIM sio watoto wa miungu bali ni
kizazi baina ya binadamu na viumbe wasio kuwa binadamu baada ya mwingiliano
wao.
BIBLIA
;
kitabi kitakatifu cha Wakristo katika Agano la Kale, wavamizi hao wametajwa
kama miungu. Wanadamu walipoanza kuongezeka katika nchi wasichana wao
wakazaliwa, wana wa Mungu wakawaona wasichana wa wanadamu ni wazuri na wakawaoa
yeyote kati yao… Mwanzo 6:1-4.
Wachunguzi wengi wa mambo
kuhusiana na kabila hilo la reptilia wanakubaliana kwamba wametokea katika
nyota ya DRACO, iliyopo baina ya
nyota saba zing’arazo sana na ambazo katika majina mengi yajulikanayo kwanza moja ni GREAT BEAR (dubu kubwa); ile iliyopo
kushoto mwa nyota hizo ni yaani kadubu kadogo (LITTLE BEAR) au NORTHERN
BEAR (yaani ALFA)
- Mapiramidi ya Misri
- Sphinx-Sanamu la Simba lenye kichwa cha binadamu liliko eneo Gaza ambalo ni la zamani zaidi kuliko mapiramidi yenyewe.
- Sanamu la Angkor Wat-Hili lipo Kambodia na mengine kama hayo nchini JAPAN
YALIYOJENGWA kwa ustadi mkubwa
wa ELIMU YA NYOTA, elimu ya maumbo na sayansi ya hali ya juu yaani ASTRONOMY, GEOMETRY na SCIENCE.
Aidha yamejengwa moja kwa moja
kwa kufuata uelekeo wa DRACO. Hata
hivyo wachunguzi wengeine pia wa mambo wanadai kwamba kabila hilo la Reptilia,
liliishi katika mashimo na mapango na inawezekana ndipo walipotokea.