INATOKA PART II
Anasema alifanya kazi hiyo kuanzia mwaka 1990 mpaka 2003 na ndipo walipo hamia mkoani tabora, baada ya mumewake kupata uhamisho wa kikazi.
Anasema alifanya kazi hiyo kuanzia mwaka 1990 mpaka 2003 na ndipo walipo hamia mkoani tabora, baada ya mumewake kupata uhamisho wa kikazi.
Anasimulia kuwa wakati akiwa mkoani tabora aliendelea na kazi
yake ya kufundisha utengenezaji wa batiki, safari hii akiwafundisha hata
waumini wa madehebu ya kiislamu pamoja na wapagani.
Alifungua duka kubwa la batiki na nguo
aina zote kama vile suruari ,mashati, vitambaa vya suti, vitenge vya
waksi, magauni ya akina mama, watoto nk ikiwa
ni utoaji huduma kwa jamii.
Alisema mwezi aprili mwaka 2009 wakati akiwa safarini mkoani
mbeya kumuuguza mama mkwe wake , alipewa taarifa na wafanyakazi wake kwamba
majambazi wamevunja duka na kuiba kila kitu.
Alisema kuwa pamoja na kupata
taarifa hizo lakini hakufadhaika sana kwa sababu alimtegemea sana mwenyezi
mungu , kwamba atamrudishia zaidi ya vile vyote vilivyopotea.
Mwaka 2010 selina alijifunza utengenezaji wa sabuni za kuogea
na kufulia za miche na za maji.
Alimtaja mwalimu wake kwa jina la elbariki mchau kuwa ndiye
aliyemfundisha kutengeneza sabuni za aina mbalimbali , pamoja na somo la
biashara la kujua faida na hasara.
Pia alimfundisha kutumia vitabu vya aina mbalimbali vya
kupokelea na kutoa , na kumwelekeza
jinsi ya kusajili biashara.
MAKALA PART III BOFYA HAPA