Elimtaa na Mjasiliamali Part II

INATOKA PART II
 
Anasema alifanya kazi hiyo kuanzia  mwaka 1990 mpaka 2003 na ndipo walipo hamia mkoani tabora, baada ya mumewake kupata uhamisho wa kikazi.

Anasimulia kuwa wakati akiwa mkoani tabora aliendelea na kazi yake ya kufundisha utengenezaji wa batiki, safari hii akiwafundisha hata waumini wa madehebu ya kiislamu pamoja na wapagani.

Alifungua duka kubwa la batiki na  nguo  aina zote kama vile suruari ,mashati, vitambaa vya suti, vitenge vya waksi, magauni ya akina mama, watoto nk ikiwa  ni utoaji huduma kwa jamii.

Alisema mwezi aprili mwaka 2009 wakati akiwa safarini mkoani mbeya kumuuguza mama mkwe wake , alipewa taarifa na wafanyakazi wake kwamba majambazi wamevunja duka na kuiba kila kitu.

Alisema kuwa pamoja na kupata  taarifa hizo lakini hakufadhaika sana kwa sababu alimtegemea sana mwenyezi mungu , kwamba atamrudishia zaidi ya vile vyote vilivyopotea.

Mwaka 2010 selina alijifunza utengenezaji wa sabuni za kuogea na kufulia za miche na za maji.

Alimtaja mwalimu wake kwa jina la elbariki mchau kuwa ndiye aliyemfundisha kutengeneza sabuni za aina mbalimbali , pamoja na somo la biashara la kujua faida na hasara.

Pia alimfundisha kutumia vitabu vya aina mbalimbali vya kupokelea na kutoa , na kumwelekeza  jinsi ya kusajili biashara.


MAKALA PART  III BOFYA HAPA