BARIDI NJOMBE NA MAKAMBAKO HADI UKUNGU
Hali ya hewa ni moja ya vitu ambavyo hupelekea watu kusafiri toka eneo
moja kwenda jingine kwa lengo la kukwepa hali flani au kuifuata hali ya
hewa ya namna fulani. Kwa nchi nyingi za magharibi, watu wengi hupenda
kusafiri mbali na wanapoishi ifikiapo kipindi cha majira ya joto. na
baadhi yao hufanya hivyo kipindi cha baridi kali. Hali ya hewa ni
kipengele muhimu kukifahamu unapopanga safari yako kwenda eneo flani
hususan safari ya mapumziko. hali ya hewa inaweza kukulazimisha
kutofanya shughuli ambazo ungependelea. mathalan, eneo linapokuwa lipo
ktk kipindi cha mvua, shughuli zinazohusisha matembezi zinakuwa ngumu
kuzifanya. ufikapo msimu wa baridi, maeneo mengine huwa na baridi kali
kiasi cha kufanya maisha kuwa kero badala ya mapumziko kwa wewe
usiyeizoea hali ya pale.
Kwa hapa Tanzania, maeneo ya nyanda za juu kusini yanafahamika kwa kuwa
na baridi kali. hali iliyopeleka mpaka wajanja kuliita baridi 'Mufindi'
- moja ya maeneo yaliyopo nyanda hizo. Hivi majuzi nikiwa njiani
kurudi dar mida ya asubuhi tulipita maeneo ya Njombe na makambako
tukitokea mkoani Ruvuma. Mtundiko huu una baadhi ya picha nilizobahatika
kupiga tukiwa njiani maeneo ya Njombe hadi Makambako ambapo tulikutana
na ukungu mzito. Kuna sehemu ukungu ulikuwa ni mwingi kiasi cha
kutulazimisha kupunguza mwendo kasi kwa kiasi kikubwa na kuwasha
indicator za hazard kuepusha maafa ya namna yoyote ile.picha ya kwanza
na ya pili ni maeneo kabla ya kufika Njombe Mjini ukiwa unatokea Songea.