Elimtaa Tv: Mimba 63 Mkoa wa Njombe ni shule za msingi na Sekondari

WANAFUNZI 62 wa shule za sekondari na msingi mkoani Njombe wamebainika wanaujauzito, wakuu wa shule mkoani humo wametakiwa kuwapima wanafunzi wao kwa kuwashitukiza ili kuwatio hofu wanafunzi kujiusisha na mahusiani.

Takwimu hizo zinatolewa na afisa elimu taaluma mkoa wa Njombe, Ambaye amesama kuwa wanafunzi 53 ni wa sekondari na tisa ni wa shule ya Msingi na kutoa maagizo ya kuwapima wanafunzi kwa kushitukia ili wananzi kuwa na woga wa kujihusisha na mahusiao huku bwazazi nao wakitakiwa kutoa ushirikiano.
Wakuu wa shule wanasema kuwa kuwapo kwa mabweni kunaweza kupunguza mimba kwa wanafunzi lakini wazazi nao wanatakiwa kuwalinda watoto wao na vijana kipindi cha rikizo.

Hayo yanabainika katika mkutano wa wakuu wa shule mkoa wa Njombe katika mkutano wao chini ya chama chao cha wakuu wa shule Tanzania Tahosa ambao wanasema kuwa changamoto ni kuwadhibiti wanafunzi ambao wanatoka nyumbani kuliko wa bweni.

Katika mkutano huu wa wakuu wa shule linaibuka suala la moto mashuleni ambao kwa mkoa wa njombe ni zaidi ya shule nne zimekumbwa na majanga ya moto ambako mkoa wa njombe unaagiza kila shule kuwa na vizimia moto vya mchanga na wakuu kuagizwa kutumia wataalamu katika ujenzi wa miundombinu ya umeme.