Elimtaa Tv: Kamati ya Zahanati Matalawe yavuliwa


WANANCHI wa mitaa ya Sidon a Buguruni wameishinikiza kamati ya ujenzi wa zahanati ya Matalawe inayojengwa na mitaa yote miwili kwa madai ya upotevu wa vitabu vya kukusanyia michango ya ujenzi na kusababisha zahanati hiyo kuchukuwa mda mrefu kukamilika.
Zahanati hii katika ujenzi wake umeibuka utata wa matumizi ya fedha za michango ya wadau na kusababisha wananchi kuitaka kamati hiyo kujiuzulu ili kupisha kamati nyingine.
Pamoja na kuchelewa kwa ujenzi wa Zahanati hiyo wananchi wanakuwa na wasiwasi wa gharama za ujenzi wa jingo hilo ukilinganisha na makatilio yao, huku wakihoji ni kwanini maafisa ukaguzi wa ndani wanakuja baada ya mambo kuharibika. 
Baada ya kuwapo kwa utata wa ujenzi wa zahanati hiyo kwenye matumizi ya fedha mkaguzi wa ndani akapitia matumizi yote na kubaini matatizo nane katika zahanati yakiwemo ya kutokuwapo kwa kumbukumbu sahihi za fedha.

Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa zahanati hiyo anajiuzulu nafasi yake ili kupisha wananchi kuchagua kamati nyingine kwa usimanizi na kusema haya.


Zahanati ya Matalawe ilianza kujengwa mwaka 2010 na ilikadiliwa kujengwa kwa milioni 60 wakati mpaka sasa imetumia milioni 52 na bado haijakamilika fedha hizo ni kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali huku nguvu za wananchi zikiwa hazijaingizwa.