Makambako shule ya msingi yapata madawati na vyumba viwili kutoka benki ya Posta

SHULE ya msingi Makambako ya halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe, wamekabiziwa madarasa mawili na ofisi kukiwa na madawati 50 katika madarasa hayo huku shule hiyo ikikabiliwa na upungufu madarasa na kusababisa wanafunzi kujazana katika madarasa.

Shule hiyo inamlundikano wa wanafunzi ukitofautisha na madarasa yaliyopo katika shule hiyo ambayo ipo katikati ya mji mkubwa kuliko yote mkoani Njombe.

Akipokea madawati hayo mkuu wa shule ya Makambako inaupungufu wa vyumba vya madarasa 24 ambapo watoto wa darasa la kwanza na lapili wamekuwa wakisoma kwa zam huku idadi ya waalimu ikiwa ni ileile.


Mwalimu huyo amepokea amepokea Madarasa na madawati kutoka Benki ya Posta Tanzania ambayo imewajengea Madarasa hayo kwa thamani ya Milioni 19 pamoja na madawati.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Dr. Rehema Nchimbi anakuwa ni mgeni Rasimi wakati wa kupokea dawati na vyumba hivyo vilivyo kabidhiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Posta, Letisia Lutashobya.


Shule hiyo inakabiliwa na upungufu wa vyumba hivyo kutokana na kuwapo kwa elimu bule kunako sababisha wanafunzi wengi kujitokeza kusoma.