HALMASHAURI YAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA KUJIENDESHA

HALMASHAURI ya Mji wa makambako mkoani Njombe, inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo  za kiuendeshaji tangu kuanzishwa kwake mwaka 2013.

Hayo yamebainishwa katika kikao cha cha baraza la madiwani ambapo imebainika kuwa imeshuka kimapato uwezo wa kujitegemea umepungua kutoka asilimia 18 kujitegemea na sasa imeshuka hadi asilimia 15.


Akiwasilisha taarifa katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Chesco Mfikwa, amekiri kuwepo kwa changamoto katika uendeshaji na kwamba inatokana na baadhi ya wafanyabiashara kugoma kutumia mashine za kielektroniki (EFD).

Akimwakilisha mkuu wa Mkoa katika kikao hicho Katibu wa Tawala wa Mkoa Jacson Saitabahu anatoa ushauri kwa madiwani kutoka hapo walipo  hivi sasa.

Deogtius Peter Mkaguzi mkazi wan je wa mkoa wa Njombe, akatoa ushauri  ili kukabiliana na changamoto hizo.


Angalizo likatolewa kwa watendaji kuhakikisha elimu inatolewa kwa wafanya biashara kuhakikisha watumia mashine za EFD ili kuepukana na ukwepaji wa kodi nakwamba sio hiari ni amri ya serikali na hivyo linahitaji utekelezaji.