WATATU WAFA KATIKA AJALI




WATU wamekufa papo hapo katika ajali mbalimbali zilizo tokea Mkoani Mbeya ikiwemo ya dereva bodaboda kugonga lori kwa nyumba na kufa papo hapo maeneo ya Mbalizi halmshauri ya Mbeya Mkoani hapa.

Akizungumzia ajali hizo kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani Athumani alisema kuwa katika ajali ya kwanza Dereva wa pikipiki maarufu Bodaboda, ambaye jina lake halikufahamika alifariki dunia baada ya kugonga kwa lori.

Alsema kuwa marehemu aliligonga lori lenyenamba za usajili namba T 388 BXS na Tela namba T 183 ABX ambalo lilikuwa likiendeshwa na Joseph Kisinda ambapo pikipiki hiyo ililigonga kwa nyuma.

Alisema kuwa ajali hiyo ilitokea juzi majila ya saa 10:30 jioni katika maeneo ya Mbalizi halmashauri ya Mbeya na mwili wa marehemu umehifadhiwa kati hospitali ya Ifisi liliyopo halmashauri ya Mbeya.

Alisema kuwa katika jajali ya pili gali aina ya Toyota Coster lenye namba za usajili T 561 BAJ likiendeshwa na Benard Mlimba lilimgonda Furaha Mwaipopo akiendesha baiskeli mkazi wa Vwawa ambaye ni dereva wa bodaboda.

Alisema kuwa marehemu alikuwa amempakiza mtu kwenye baiskeli na abilia wake Nione Sanga alijeruhiwa katika ajali hiyo na anapatiwa matibabu kmatika Hospitali ya Vwawa wilayani Mbozi.

Aliongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Vwawa na dereva wa gali hiyo alitoloma mara baada ya kutokea kwa ajali hiyo.

Alisema kuwa katika ajali ya tatu, Sailosi Cheyo aligonwa na Lori aina ya Fawn a kusababisha kifo chake papo hapo wakati akijalibu kuvuka barabara.

Alisema kuwa tukio hilo lilitokea katika maeneo ya kijiji cha Chimbuya Wilayani Mbozi na gali hilo lenye namba za  usajili T 509 BNP lenye tela namba T 231 BME likitokea Fingo Sijabaje mkazi wa Forest Jijini Mbeya.

Alisema kuwa ajali hiyo ilitokea mara baada ya galihiyo kuacha njia na kumvaa mtembea kwa miguu huyo na kusababisha kifo chake.