RAIS ATEUWE MAWAZIRI WALIO NA TAARIMA YA WIZARA HUSIKA


WANANCHI wakazi wa Mbalizi mkoani Mbeya wametoa maoni mbalimbali katika Rasimu ya katiba iliyotangaza hivi karibuni wakitaka raisi atangazwe baada ya kushinda kwa saidi ya asilimia 50.
 
Hayo yamebainishwa Juzi katika mkutano mapitio ya rasimu ya katiba mpya  ulioandaliwa na Asasi ya Hope for Deprived Action in Deveropment (HDPAD), na kufanyika nje kidogo ya mjimdogo wa Mbalizi na kuhusisha zaidi ya wakazi 80 na kutoa maoniyao.

Moja ya kundi la washiliki katika  mkutano huo walipengekeza kuwa Rais atatangazwa kuwa mshindi pale tu atakapo fanikiwa kufukisha kula zaidi ya asilimia 50 ya kula zite zitakazo pigwa.

Kudi hilo likiongozwa na Eliud Mwambope alisema kuwa Mwambope akizungumza kwa niaba ya kundi alisema kuwa kundi lake limependekeza kuwa raisi atatangazwa kuwa ameshinda mpaka atakapo onekana amefikisha zaidi ya asilimia 50 ya kura zote za washiliki.

alisema kuwa ikitokea mgombea anaye ongoza hajafikisha asilimia 50 inatakiwa uchaguzi uludiwe na Yule anaye mfuata ile sheria ya ‘simple majority’ iondolewe.

“Tumependekeza kuwa Rais atatangazwa kuwa ni Mshindi baada ya kushinda kwa zaidi ya asilimia 50 ikitokea hakuna aliyefikisha basi walio fuatana katika uchaguzi huo warudie uchaguzi  ile sheria ya Simple majority iondolewe” Alisema  

Pia katika uteuzi wa mawaziri Rais ateuwe mawaziri kulingana na taaluma ya anaye teuliwa ili ufanisi katika utendaji kazi wa mawaziri.
Hivyo katika katiba mpya kuwepo na kipengele kinacho mrazimu raisi kuteuwa mawazili walio na taaruma ya wizara husika.

Rasimu ya katiba mpya imeendelea kujadiliwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini kupitia mabaraza ya katiba waliyoandaliwa na taasisi mbalimbali.