MBEYA CITY WAMLAZA RUVU SHOTING 2-1




TIMU ya Mbeya City imeitunishia misuli timu ya Ruvu Shoting kwa kuichapa mabao 2-1 wakewa wenyeji wao mkoani Mbeya.

Meshihoyo ambayo imechezwa katika viwanja vya Sokoine jijini Mbeya Mbeya City ikiwa mwenyeji wa Timu ya Ruvu Shoting, ilianza kwa kutikiza nyavu za goli la mgeni wake katika dakika ya 8 katika kipindi cha kwanza kupitia mchezaji wa timu hiyo John Kabanda.

KIKOASI CHA MBEYA CITY

MBEYA CITY WAKISHANGILIA USHINDI WA GOLI LA PILI

KOCHA WA TIMU YA MBEYA CITY JUMA MWAMBUSI



Goli hilo la Mbeya city lilidumu kwa 13 kabla ya timu hiyo kusawazisha katika dakika ya 25 ambapo ilitokea piga nikupige katika timu ya Mbeya city na kumaliziwa na Paul Nonga.
Hadi dakika 45 zinamalizika timu hizo zilikuwa zimetoshana ubavu kwa kuwa na sale ya goli moja kwa moja.
MSEMAJI WA MBEYA CITY FREDY JACKSON a.k.a FREDOO

CHARLES MKWASA KOCHA WA TIMU YA RUVU SHOTING
Timu ya Mbeya City ambayo kwanza ndo inaingia katika mtanange wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania haikulizika na sale wakiwa nyumbani ambapo ilipo fika dakika ya 90 ya mchzo huo Stive Mazanda hakulizika na sale hiyo na kisha kutikisa nyavu za mpinzani wake kwa kuutupia mpira golini.

Hadi mpira unamalizika timu ya Mbeya City imeibuka kifuambele kwa ushindi wa bao 2-1 huku Ruvu Shoting waki ondoka kichwa chini.

Nae kocha wa Timu ya  Ruvu Shoting Charles  Mkwasa alisema kuwa ushindi wa Mbeya City ni waharali ila amemlalamikia muamuzi kwa kumaliza mpira kabla ya Dakika 5 za nyongeza kumalizika mara baada ya timu yake kufungwa goli la pili.

Kwa upande wake Juma Mwambusi Kocha wa Timu ya Mbeya City amewataka mashabiki wa timu yake kuwa wavumilivu timu iwapo uwanjani.

Mwambusi amewataka mashabiki kuachana na lugha za matusi kwa wachezaji na kuacha mpaka mpira umalizike kwani kwa kufanya hivyo wanawakatisha tama wachezaji.

Timu ya Mbeya City huu ni ushindi wake wa Kwanza toka iingie katika ligi hii ambapo katika ambapo katika mchezo wa kwanza walifurukuka kwa kutoana jasho na timu ya Kagera sugar.

STORY PICHA NA  HABARI ONLINE